Jinsi Maulid Kitenge alivyomnusuru Nape na bastola MUUNGWANA BLOG / 3 hours ago MWANDISHI wa habari, Maulid Kitenge, ambaye juzi alimnusuru aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye dhidi ya mtu aliyemshikia bastola wakati akielekea kuzungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Protea, jijini Dar es Salaam, amefunguka na kueleza kile kilichomsukuma aingilie kati. Juzi, mara baada ya Nape kuwasili karibu na hoteli hiyo, ambayo inapakana na Kanisa la Mtakatifu Petro, lililoko eneo la Oysterbay, aliposhuka tu ghafla kijana huyo mrefu mweusi akiwa amevalia suruali ya jinzi, shati la mikono mirefu la mistari mistari pamoja na kofia, alimkimbilia na kumshika mkono kiongozi huyo akimtaka arudi kwenye gari. Nape hakukubaliana na hatua hiyo, ambaye alimtaka kijana huyo aonyeshe kitambulisho, lakini hakufanya hivyo, zaidi alirudi hatua chache nyuma na kisha kutoa bastola iliyokuwa kiunoni kwake na kumtishia. Wakati tukio hilo likitokea, ghafla alitokea k...
Maoni
Chapisha Maoni